Thursday, January 28, 2016

Staa wa tennis duniani kwenye fainali za Austalian Open


Novak Djokovic amefuzu kucheza fainali ya mashindano ya tenisi ya Australian Open kwa mara ya sita baada ya kumfunga Roger Federer.

 
Mchezaji huyo anayeshika nafasi ya kwanza kwa ubora duniani amepata ushindi wa 6-1 6-2 3-6 6-3.
Djokovic atakutana mshindi kati ya Mwingereza Andy Murray au raia wa Canada Milos Raonic kwenye fainali.
Mserbia huyo tayari amemshinda Murray kwenye fainali mara tatu ikiwa ni pamoja na mwaka jana aliposhinda kwa seti nne.


No comments:

Post a Comment