Siku ya leo Idris ameweza kuwashukuru Wabongo kwa kumpigia kura kipindi yupo kwenye jumba la BBA na baadae atafanya tour kwa baadhi ya nchi kwa ajili ya kuwashukuru watu wote kwa kumpigia na hapa akifunguka zaidi.
“Naomba nitoe shukrani zangu kwa Wabongo wote coz tangu nafika napewa hongera sana ila na mimi nawapa Hongera sana nyinyi kwasababu mlifanyakazi kubwa sana mimi nilikuwa nalala tu, all in all nawapa hongera sana kwa kuni-support vya kutosha ingawa nilipata kula tano ila naamini wote walinipigia kura ushindi wangu ulikuwa mkubwa sana yote ilitokana na nyinyi Watanzania.
Ndio maana nilivyotangazwa kuwa ni mshindi niliulizwa kuwa nitazifanyia nini hizo hela nikawajibu ushindi wangu
naurudisha kwa Wabongo watu wakawa na controversial may be nitarudhisha mkwanja bali ni effort, nguvu, upendo walizozitumia kwangu.”


No comments:
Post a Comment