Baada ya jana Diamond Platnumz kufunguka yake kwenye kipindi cha XXL
cha Clouds Fm juu ya beef linaloendelea kati yake na mwanamuziki Ommy Dimpoz kuhusu vijembe vyao vya kupumuliwa na kununua viewers. Leo ilikuwa zamu ya Ommy Dimpoz kufunguka soma hapa.
“Nilipopost 'insta' kuhusu watu kununua 'views' YouTube,
sikumtaja mtu, nilisema tu sasa hivi watu wanaweza kununua 'views', nafikiri
sio kitu kizuri kwa sababu utakuwa unajidanganya unajitekenya huku unacheka
mwenyewe, kwa sababu kuna jamaa alishawahi kunicheki kuhusu ishu hiyo, video
yangu ya Wanjera ilikuwa na views laki tisa na laki nne ilikuwa imekaa mwaka
mzima, akaniambia naweza kununua views nikamwambia kivipi, akaniambia nimtumie
link baada ya masaa matano ikawa na views.
Baada ya kupost 'insta' kuwa kuna wasanii wananunua 'views'
YouTube, nilikutana na meneja wa Diamond, Sallam akaniambia hakuna kitu ulichoniudhi
kama kuongelea suala la views, nkamwambia kivipi akasema lazima utakuwa
unamzungumzia Diamond, sijiamini, mara kwenye mtandao wakaanza kusema nina wivu.
Ukweli sikutaka kuongea kitu chochote, hata kwenye interview zangu
sikutaka kuzungumzia 'ugomvi' wangu na Diamond, kwa sababu nilikuwa
nikiamini ni upepo mbaya tu utapita, na mambo mengine yanaweza kuendelea
mkapatana, mbona kuna watu wanagombana na Baba zao sembuse sisi, lakini
vyanzo zilikuwa ni vingi sana, ushikaji wangu mimi na Diamond haujaanza
leo, tangu naimba Top Band, hajatoa hata Nenda Kamwambie, alishawahi
kuniambia watu wanataka nigombane naye ili asinipeleke kwa
mganga wake, nikamwambia asiwajali hao wanaosema hivyo afanye kazi yake
na isiharibu ushkaji wetu, lakini niwaka naona kadri siku zilivyokuwa
zinakwenda mwenzangu alikuwa kama ananikwepa, kuna kipindi nilikuwa
siwezi kufanya kitu chochote bila kumwambia yeye, wakati natoa Tupogo
nilimsikilizisha akaniambia iko poa, nkamwambia nataka nmlete King Maluu
aje kupiga saxophone kwenye hii nyimbo, cha kushangaza baada ya wiki
nimepita zangu studio kwa Mackochalli namkuta Diamond na King Maluu
anapiga saxophone kwenye wimbo wa Number One, alishtuka sana."
Bdozen: Je tangu muwe marafiki na Diamond vitu gani uliwahi
kuvichangia kwake…?
Ommy Dimpoz: Mimi sijawahi kusema sehemu yyt ila hili ndio mara yangu ya
kwanza nalisema Ngoma ya nasema nawe ya diamond niuandishi wangu ila sijawahi
ata siku moja kusema nimeandika mimi

No comments:
Post a Comment