Matokeo hayo hayamaanishi kwamba ugonjwa huo unaweza kusambazwa kupitia maji maji hayo ya mwilini.Sababu kuu ya kuenea kwa virusi hivyo ni kupitia kuumwa na mbu,lakini wanasayansi wanachunguza njia nyengine.
Huku maambukizi ya Zika yakiwa sio makali,ugonjwa huo umehusishwa na maelfu ya watoto waliozaliwa na kasoro.
Paula Gadelha,mkuu wa taasisi ya Fiocruz ambayo inashirikiana na wizara ya Afya amesema:''Virusi hivyo vya Zika vimepatikana katika Mate na mikojo''.
''Lakini hiyo hainamishi kwamba kuna uwezekano wa kuenea kwa virusi hivyo kupitia mate na mikojo.Hatari ya kuenezwa kwa virusi hivyo kupitia maji maji ya mwilini uliangaziwa nchini Marekani ambapo kituo cha udhibiti wa magonjwa kinaamini kisa kimoja kilisambazwa kupitia ngono''.
Hatahivyo kumekuwa na kesi mbili pekee za usambazaji wa virusi hivyo kupitia ngono.

No comments:
Post a Comment