Sexy lady wa Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’.
Safari hii ndiyo basi tena! Pamoja na
kujishaua mbele ya kamera za wanahabari na simu za kuteleza (smart
phones) kisha kutupia kwenye mitandao ya kijamii wakizuga wapo pamoja,
habari ya mjini inadai kwamba, sexy lady wa Bongo Movies, Wema Isaac
Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ amemmwaga staa wa Ngoma ya Mdogomdogo, Nasibu
Abdul ‘Diamond Platnumz’.Kwa mujibu wa chanzo makini ambacho ni rafiki
mkubwa wa wapenzi hao, ishu ya kumwagana ilikuwepo muda mrefu lakini
kinachoendelea ni kuwazuga mashabiki wao ili wasishuke kisanaa.
SAFARI YA CHINA
Chanzo hicho kilifunguka kwamba, siku
chache zilizopita Wema au Madam kama anavyopenda kuitwa, alimwambia
Diamond kuwa anakwenda China kuchukua mzigo bila kumwambia ni mzigo gani
na kwamba huko aliambatana na wanaume wanne, wawili wakiwa ni Martin
Kadinda na Petit Man.
KAMA MBWAI, IWE MBWAI
Ilidaiwa kwamba wanaume wengine
wawili wapo kwenye mabano, jambo ambalo Diamond au Dangote kama
anavyopenda kujiita, hakuliafiki suala hilo lakini Madam akasema liwalo
na liwe yaani kama ‘mbwai iwe mbwai’ hivyo akampuuza na kwenda zake
China!
AHADI HEWA? UBAHILI WAMPONZA DIAMOND
Chanzo hicho kiliendelea kumwaga
‘ubuyu’ kwamba, tabia ya Diamond ya ubahili, nayo imechangia kwa Wema
kukaa pembeni kwani jamaa huyo siyo mkataji wa mkwanja kama ilivyokuwa
kwa yule kigogo wa Wema, Clement.
No comments:
Post a Comment