Monday, October 27, 2014

BOB JUNIOR ATUA HAPA SASA


Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Sabby ambaye ndiye aliyevujisha picha za tukio hilo, Sabby na Bob Junior kwa sasa wako katika mahaba mazito na ni watu wanaopendana kwa sababu kila unapomuona Sabby yupo karibu na mwanamuziki huyo.
“Sasa hivi Sabby na Raheem ndiyo habari ya mjini kwani kila sehemu wapo pamoja na wanapendana sana,” alidai rafiki huyo wa Sabby.Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba wawili hao wanaweza kuvalishana pete ya uchumba muda wowote kuanzia sasa.
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Bob Junior ambaye hakupatikana lakini alipotafutwa Sabby ili kusikia kauli yake kuhusu uhusiano wake na Bob Junior alikiri na kusema kuwa ni mtu ambaye anampenda na ndiye anamfanya awe na furaha.
























Source: GPL

No comments:

Post a Comment