Kwa mujibu wa rafiki wa karibu wa Sabby
ambaye ndiye aliyevujisha picha za tukio hilo, Sabby na Bob Junior kwa
sasa wako katika mahaba mazito na ni watu wanaopendana kwa sababu kila
unapomuona Sabby yupo karibu na mwanamuziki huyo.
“Sasa hivi Sabby na Raheem ndiyo habari ya
mjini kwani kila sehemu wapo pamoja na wanapendana sana,” alidai rafiki
huyo wa Sabby.Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba wawili hao
wanaweza kuvalishana pete ya uchumba muda wowote kuanzia sasa.
Baada ya kunyetishiwa ubuyu huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Bob
Junior ambaye hakupatikana lakini alipotafutwa Sabby ili kusikia kauli
yake kuhusu uhusiano wake na Bob Junior alikiri na kusema kuwa ni mtu
ambaye anampenda na ndiye anamfanya awe na furaha.Source: GPL



No comments:
Post a Comment