Friday, January 16, 2015

CHRIS BROWN ACHUNGULIA JELA

Mwanamuziki wa R&B, Chris Brown amerudishwa tena mahakamani baada ya kushindwa kutekeleza majukumu aliyopewa kwa ajili ya maangalizo kipindi alipokumbwa na kesi ya kumpiga ex-girl friend wake 'Rihanna' mwaka 2009.


Mahakama ya Los Angeles kupitia kwa jaji James Brandlin alimuachia huru mwanamuziki huyo kwa ajili ya kutekeleza yale aliyopewa na mahakama kama kujumuika katika majukumu ya kijamii na kutoondoka bila kutoa taarifa, kwa mujibu wa mtandao wa Mailonline umeripoti kuwa mwanamuziki huyo halishindwa kutimiza majukumu aliyoangizwa na mahakama kwa wakati, kwasasa Cris yupo huru hadi mwezi wa nne tarehe 20 na hakimu anategemea majibu kutoka kwa wasimamizi wake wanaomfatilia.

No comments:

Post a Comment